Adverts

Showing posts with label Bongo Movie. Show all posts
Showing posts with label Bongo Movie. Show all posts

Friday, August 26, 2016

Wasanii Wapenda Amani Waungana Kupinga Maandamano UKUTA Ya Chadema


WASANII mbalimbali wanaopenda amani wameungana kwa pamoja kupinga maandamano ya UKUTA yanayotarajiwa kufanyika Septemba Mosi, mwaka huu.
 
Akizungumza jana mbele ya Waandishi wa Habari, Mwenyekiti wa Wasanii hao wapenda amani, Steve Nyerere alisema hamna haja ya maandamano bali tunahaja ya kufanya kazi hususan kwa vijana.
 
"Vijana ndio muhimili mkubwa kulinda amani ya nchi,tusiwaze maandamano bali tuwaze je Akinamama na Watoto wanapata huduma hospitali"alihoji Steve Nyerere.
 
Kwa Upande wa Makamu Mwenyekiti wa Wasanii hao, Asha Baraka alisema wameamua kupaza sauti zao kwa niaba ya Wasanii wote wanaopenda amani.
 
Alisema Tanzania ni nchi ya Amani sio nchi ya vita hivyo wanapofanya shughuli za UKUTA shughuli zote za kijamii zitasimama.
 
Hatahivyo aliomba Septemba 1,  UKUTA wasimamishe maandamano hayo, pia watafute njia muafaka ya kuweza kuongea Vyama kwa Vyama na wakapata muafaka ili nchi iweze kwenda mbele.

Sunday, March 20, 2016

Kichanga Mwingine Adaiwa Kufariki Dunia Kwa Uzembe Mkoani Mwanza


Matukio ya wajawazito kupoteza watoto kwa madai ya uzembe wa wahudumu wa afya yameendelea kuugubika Mkoa wa Mwanza baada ya mkazi wa Nyarawambo wilayani Sengerema Tatu Muhangwa, kujifungua na mtoto wake kufariki kwa kukosa huduma.

Mama mzazi wa Tatu, Vumilia Nailon alisema mjukuu wake alifariki baada ya wahudumu wa afya katika Zahanati ya Ngoma ‘B’ iliyopo Kata ya Nyamatongo wilayani Sengerema, kuchelewa kumhudumia.

Mhudumu wa afya aliyekuwa zamu, Helena Mulwisha alisema alishindwa kumhudumia mjamzito huyo kutokana na kubaini kuwa mtoto alikuwa kakaa vibaya tumboni na kuwashauri kumpeleka hospitali ya wilaya kwa msaada zaidi.

Nailon alisema: “Nilimfikisha mgonjwa wangu zahanati juzi, saa kumi na moja alfajiri, lakini hadi saa tatu hakuwa amepatiwa huduma yoyote hadi alipojifungua mwenyewe bila msaada na mtoto kufariki.

“Mmoja wa wahudumu wa afya aliyekuwapo alishindwa kumhudumia baada ya kugundua mtoto amekaa vibaya tumboni na yeye hana utaalamu wa kumsaidia.”

Alisema Mulwisha aliwashauri kumpeleka mgonjwa hospitali ya wilaya kwa sababu wauguzi na madaktari walikuwa wakihudhuria semina.

“Baada ya kukosa gari ya kumuwaisha hospitali, tuliamua kutembea kwa miguu umbali wa kilomita mbili, lakini hatukufika baada ya magonjwa wangu kujifungulia njia kwa msaada wa wasamaria wema na mtoto kufariki,” alisema Vumilia.

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Dk Henry Nyamete alisema ofisi yake inachunguza tukio hilo na kwamba itachukua hatua za kinidhamu dhidi ya mhudumu wa afya aliyekuwa zamu siku hiyo kwa kushindwa kuwajibika kwa kuita gari la wagonjwa ili kumuwahisha mjamzito huyo hospitali kwa matibabu zaidi.

Wednesday, March 16, 2016

Taarifa ya Wizara kuhusu filamu iliyompatia tuzo Elizabeth Michael "Lulu"

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kumekuwa na minongono mingi kutoka kwa baadhi ya wananchi kuhusu Filamu ya Mapenzi ya Mungu ya msanii Elizabeth Michael (Lulu) iliyoshinda tuzo ya Filamu bora Afrika Mashariki mapema mwezi huu huko Lagos Nchini Nigeria katika tuzo za African Magic Views Choice Award (AMVCA).

Ili filamu ikamilike inahusisha watu mbalimbali wanaoshirikishwa kukamilisha filamu kuanzia mtoa wazo ambaye wazo hilo huwekwa katika mswada na mtaalamu jambo ambalo haliondoshi umiliki wa filamu.

Tunapenda kuufahamisha umma kuwa mmiliki halali wa Filamu ya Mapenzi ya Mungu ni Msanii Elizabeth Michael (Lulu) na ndiye aliyepata tuzo kwani ana haki zote za kupata tuzo hiyo kama mmiliki halali wa filamu hiyo.

Filamu ya Mapenzi ya Mungu imetengenezwa chini ya kampuni ya Proin Promotion na imesajiliwa kwa namba ya usajili CO831190.

IMETOLEWA NA
WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO